• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga
Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Eneo la Utawala
    • Majukumu ya Viongozi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi na Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Radio Ulanga FM
      • Ijue Radio Ulanga FM
      • Vipindi vya Radio Ulanga FM

Wananchi wa wilaya ya Ulanga waelezea uhalisia wa Mradi wa Urasimishaji Ardhi

Imetumwa: June 9th, 2019

ULANGA

 

NA FATUMA MTEMANGANI

Mradi wa urasimishaji wa Ardhi,Land Tenure Support Programme [LTSP] umeleta mafanikio kwa kuleta mpango wa matumizi bora ya Ardhi kwa kutenga maeneo ya kijamii,upimaji wa mashamba,kujenga uelewa wa masuala ya Ardhi kwa wananchi wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro.

Akizungumza katika mdahalo wa uhalisia wa mradi huo afisa Ardhi wa wilaya ya Ulanga bwana Vallenc Huruma amesema kuwa,mradi huo pia umeondoa migogoro baina ya wakulima na wafugaji,wakulima na Hifadhi ya Selous,kijiji na kijiji,wakulima kwa wakulima pamoja na kijiji na wananchi.

Bwana Vallenc aliongeza kuwa mradi pia umesaidia kuongeza thamani ya Ardhi ikiwemo uuzwaji holela wa Ardhi pamoja na jamii kutoharibu vyanzo vya maji kwa kufuata sheria mama ya mazingira na kuhifadhi misitu ya vizuri,kufanya usafi na ulinzi kwenye misitu yao ya vijiji,kwani dhima ya serikali kwenye hati miliki ya kimila ni mwananchi kujua miliki ya kipande chake cha Ardhi na kumuondolea migogoro ya mipaka baina yake na jirani yake.

“Migogoro ya Ardhi kwa sasa wilaya ya Ulanga imepungua kabisa hasa kwa jamii ya wafugaji tofauti na hapo awali ambapo ofisi yangu ilikuwa ikipokea kesi nyingi lakini kwa sasa hakuna kesi yeyote inayoletwa kwenye ofis yangu na pia jamii imeelimika juu ya matumizi bora ya Ardhi kwa kutenga maeneno ya makazi,makaburi,shule,ofisi za vijiji,Taasisi,eneo la malisho na kilimo”.Alisema Vallenc Huruma

Pia mradi umewajengea uwezo vyombo vya utatuzi wa migogoro ya Ardhi ikiwemo mabaraza ya Ardhi ya vijiji na mabaraza ya kata kwa wilaya ya Ulanga,pia kuwajengea uwezo misaada ya kisheria kwa wanawake kujua haki ya kumiliki Ardhi kupata mirathi ya Ardhi kwa mume wake hata kwa familia ya wazazi wake kupitia chama cha sheria cha wanawake Tanzani [TAWLA].

“kwanza nawashukuru sana wananchi hao kutambua nini maana ya mradi na unafanya nini katika vijiji vyao,kwa uelewa huo naamini mpango wa matumizi bora ya Ardhi utafanyia kwa kufuata sheria na taratibu zilizowekwa”Alisema Vallenc.

Aidha umesaidia kukarabati ofisi za masijala ya Ardhi,umeshawishi wa kujengwa baraza la Ardhi la wilaya na umeanza rasmi kwa uwekaji wa alama na upimaji unaotumika ni kupima kwa kutumia teknolojia rafiki kabisa hivyo ameataka wananchi wasiopima mashamba yao kwenye maeneo yao kwani mradi ukimaliza muda wake mwananchi atapimiwa kwa gharama yake.

Kwa wilaya ya Ulanga mradi wa urasimishaji Ardhi umelenga kufikia vijiji 52 kwa wilaya ya Ulanga hivyo mpaka sasa tayari mradi umefanya kazi katika vijiji 40 bado vijiji 12 hii ni kutokana na changamoto ya mvua zilizokuwa zinaendelea kunyesha wilayani Ulanga kuharibu miundombinu ya barabara na mashamba kujaa maji hali iliyosababisha kusimama kwa zoezi la upimaji wa mashamba katika vijiji vilivyosalia.

Baadhi ya wananchi wameelezea uhalisia wa mradi huo ulivyowasaidia wanawake kuwa na hati miliki za kimila kwa kuwainua wanawake kiuchumi kupitia Ardhi zao wenyewe kwenye ndoa zao na hata family ya wazazi wake.

Wananchi hao wameiomba ofisi ya Ardhi kuwaongezea thamani ya hati miliki ya kimila lengo likiwa ni kujikwamua kiuchumi,na mradi utapoisha wataalam wa LTSP waongezewe muda wa kubaki Ulanga kuwasidia wananchi kusimamia kupima maeneo yaliyobaki ili kusiwe na migogoro inayowahusu wananchi.

Mradi wa urasimishaji wa Ardhi,Land Tenure Support Programme [LTSP] kwa wilaya ya Ulanga unatarajia kukamilika tarehe 30/6/2019 hivyo zoezi la upumaji litaendelea kwa vijiji 12 vilivyobaki mpaka mradi utakpokamilika kwa wakati

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA ULANGA October 04, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI November 22, 2021
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA MFUMO WA ANUANI ZA MAKAZI TARAFA YA VIGOI March 14, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI YA MWAKA 2022 May 06, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Hakimu mfawidhi Ulanga atambulisha wiki ya sheria

    January 17, 2024
  • Hakimu mfawidhi Ulanga atambulisha wiki ya sheria

    January 17, 2024
  • Bonanza la Uhuru lafana Ulanga

    December 08, 2023
  • Kuelekea Siku ya 9 December Viongozi na Wananchi wa Wilaya ya Ulanga wafanya usafi katika Hospital ya Wilaya

    December 06, 2023
  • Angalia Zaidi

Video

Link Kuripoti shuleni
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Vipindi vya Radio Ulanga
  • Majukumu ya Viongozi wa Serikali za Mitaa
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA FFARS
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

    Anwani ya Posta: P.O. BOX 22

    Telephone: +2550232626340

    Simu: 0763845957

    Barua pepe: ded@ulangadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2017 Ulanga District Council . All rights reserved.