• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga
Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Eneo la Utawala
    • Majukumu ya Viongozi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi na Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Radio Ulanga FM
      • Ijue Radio Ulanga FM
      • Vipindi vya Radio Ulanga FM

Maji

HALMASHAURI YA WILAYA YA ULANGA

IDARA YA MAJI

1.0 UTANGULIZI

 Idara ya maji ni moja kati ya Idara 12 za Halmashauri ya Ulanga na ilianzishwa rasmi tangu serikali ilipoamua kurudisha madaraka na majukumu katika ngazi ya Serikali za Mitaa mwaka 1984.

2. Hali ya watumishi

Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga katika idara ya maji ina jumla ya watumishi 8 kati ya watumishi 28 wanaohitajika kulingana na mapendekezo ya Wizara ya Maji. Watumishi waliopo wako katika maeneo mawili ambayo ni Idara ya Huduma ya maji Kijamii na Idara ya Huduma ya Maji Kibiashara;

Huduma ya maji Kijamii

Na
Watumishi/kundi
Ngazi ya elimu
Idadi
1
Mhandisi wa maji
Degree
1
2
Fundi sanifu
Form IV
1
3
Fundi sanifu
Diploma
1
4
Fundi sanifu wasaidizi ngazi ya Trade test
STV VII ( trade test)
1


Jumla
4

 Huduma ya Maji Kibiashara

Na
Watumishi/kundi
Ngazi ya elimu
Idadi
1
Fundi sanifu
Form IV
1
2
Fundi sanifu wasaidizi ngazi ya Trade test
STV VII ( trade test)
3


Jumla
4

3.0 HALI YA HUDUMA YA MAJI

Miongozo na sera mbalimbali

Usimamizi na mipango yote ya utoaji wa huduma ya maji kwa wananchi inazingatia misingi muhimu ifuatayo.

· Sera ya Taifa ya maji 2002.

· Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025.

· Malengo ya Milenia.

· Ilani ya uchaguzi chama Tawala (CCM) 2015

· Miongozo mbalimbali inayotolewa na serikali kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo.

· Mkakati wa kupunguza umaskini na kukuza uchumi (MKUKUTA).

 

 3.1 VYANZO VYA MAJI

Wilaya Ulanga inahudumia Wananchi maji kutoka kwenye vyanzo vya maji ambavyo hutokana na Mito, chemichemi na visima virefu.

Hali ya mazingira ya vyanzo vya maji bado ni ya kuridhisha kwani vyanzo vyote bado vinaendelea kutoa maji japokuwa kuna changamoto ya kupungua kwa baadhi ya vyanzo kulingana na mabadiliko ya hali ya hewa na tabia ya nchi.

 

3.2 HALI YA UPATIKANAJI WA HUDUMA YA MAJI

Hali ya upatikanaji wa maji kwa wingi na ubora katika wilaya ni ya wastani ambapo huduma inapatikana kwa kiwango cha asilimia 59 ya wakazi wake .Aidha kuna visima vifupi vya maji vipatavyo 285, visima virefu 12 na skimu 9 za maji ya bomba zinazoendeshwa na kumilikiwa na wananchi kupitia Jumuiya za Watumiaji Maji na Bodi ya maji.

 

3.3 UBORA WA MAJI

Katika kuhakikisha kuwa usalama wa maji unaendelea kuwepo ,uchunguzi wa ubora wa maji unafanyika kabla ya mradi haujajengwa. Na zoezi la kutibu maji hufanyika kabla ya kugawa maji kwa kutumia madawa aina ya clorine.

3.4 USHIRIKIANO NA WADAU WENGINE WA MAENDELEO

Ili kuongeza kiwango cha utoaji na upatikanaji wa huduma ya maji Halmashauri kupitia idara yake ya maji inashirikiana na wadau wengine vizuri kama Shirika lisilo la kiserikali la Solidermed, Kanisa Katoliki Jimbo la Mahenge(CARITAS) na Lions Pure Water katika kutoa huduma kupitia miradi ya maji na kutoa mafunzo kwa wananchi.

4.0 MAENDELEO YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAJI YA KATIKA 10(WSDP)

Halmashauri ya wilaya ya Ulanga inatekeleza programu ya maendeleo ya sekta ya maji katika vijiji 10 (Mgolo, Minepa, Igota/Kichangani, Nkongo, Gombe, Tanga, Ngoheranga, Lupunga, Marinyi, Kipingo na Makerere. Miradi hii inatekelezwa kwa awamu mbili. Awamu hizo ni

i) Usanifu na upembuzi wa miradi

ii) Ujenzi wa miundombinu ya maji

4.1 USANIFU WA MIRADI

Kazi ya awali katika miradi hii ilikuwa kufanya usanifu wa miradi. Aidha usanifu huu ulikuwa unategemea upatikanaji wa vyanzo vya maji kwa maeneo husika. Aina mbili ya vyanzo vya maji zilipendekezwa kutumika na wananchi kutegemea na upatikanaji wa maji kwa maeneo husika na uwezo wa wananchi katika kuendesha miradi hiyo.

Vyanzo vya maji hivyo ni :-

i) Maji ya juu ya ardhi (Mito chemchemi , mabwawa nk)

ii) Maji chini ya ardhi (Visima virefu vya maji ) au visima vifupi

4.2 MAJI YA MTO

Baadhi ya Vijiji vilichagua teknologia ya kutumia maji juu ya ardhi kwa vile kulikuwa na uwezekano wa kupata vyanzo vya maji juu ya ardhi .Vijiji vilivyochagua kutumia maji ya mto kutokana na vijiji hivyo kuwa karibu na mito ni Mgolo ,Gombe , Malinyi,Kipingo na Makerere.

 4.3 VISIMA VIREFU

Katika maeneo ambayo yaliyobainika kutokuwa vyanzo vya maji ya Mito ilipendekezwa kutumika visima virefu au vifupi.

Vijiji vya Nkongo, Gombe, Kichangani, Lupiro, Minepa, Ngoheranga na Lupunga wananchi walichagua kutumia visima virefu.

Vijiji vya Kichangani, Lupiro, Minepa na Lupunga vilifaulu kwa kupata maji na ujenzi wa miundombinu ulijengwa. Vijiji vya Nkongo, Ngoheranga na Tanga vilikoswa maji, hivyo pakafanyika utafiti wa kuchimba visima virefu kwa kila kitongoji ili kuangalia uwezekano mara ya pili badala ya mradi wa maji ya bomba.

 

 4.4 UJENZI WA MIUNDOMBINU YA MAJI

Ujenzi wa miundombinu ya maji ipo kwenye hatua mbalimbali ikiwemo kukamilika, umaliziaji na ujenzi

A. MIRADI ILIYOKAMILIKA NA HUDUMA INATOLEWA

Miradi iliyokamilika ni Lupunga, Lupiro, Igota/Kichangani na Mgolo. Ambapo miradi yote inaendeshwa na wananchi wenyewe kwa kusimamiwa Jumuiya ya Watumiaji Maji iliyosajiriwa.

Mapungufu mbalimbali ya miradi Halmashauri, mkandarasi mshauri na Mkandarasi wa ujenzi na Bodi za maji kwa pamoja tunashughulikia kwa karibu kuzikamirisha.

B. MIRADI AMBAYO IPO HATUA YA UMALIZIAJI

Mradi ambayo ipo kwenye hatua ya umaliziaji na huduma haijaanza tolewa ni mradi wa Kijiji cha Minepa, ambapo tatizo lilikuwa bomba kupasuka karibu na mtambo wa kusukumia maji. Tatizo hili limetatuliwa na sasa upo kwenye utaratibu wa kukaguliwa na kukabidhiwa wananchi

Mradi wa pili ni Gombe ambapo chanzo ni mto, maji yalishindwa kuingia kwenye tanki. Huduma ya maji ilikuwa inatolewa bila kuingia kwenye tanki. Ila kwa sasa kunaitilafu ambapo mkandarasi yupo eneo la ujenzi anarekebisha/anakarabati. Utatuzi wa kudumu tumemuomba Katibu Mkuu Wizara ya Maji atume mtaalam tushirikiane kupitia usanifu.

 C. MIRADI AMBAYO IPO HATUA YA AWALI

Miradi ambayo ipo hatua ya awali ni mradi wa maji ya bomba Marinyi, Kipingo na Makerere. Mradi wa pili ni wa uchimbaji wa visima virefu 20 Nkongo, Ngoheranga na Tanga. Ambapo wakandarasi wapo eneo la mradi wanaendelea na ujenzi.

3.5 GHARAMA ZA MRADI

Jumla ya gharama yote ya mradi wa maji ya Vijiji 10 ni Tsh 5,107,070,266.31 ambapo kiasi cha Tsh 2,164,246,008 kimepokelewa na Kimelipwa wakandarasi. Mchanganuo kwa kila mradi kama ifuatavyo;

 

Kijiji
Gharama ya Mkataba (Bila VAT)
KIASI KILICHOLIPWA (Tshs)
Kichangani

427,864,721.00

384,910,338

Igota
Lupiro

396,802,107.70

362,612,542.

Gombe

368,431,894

348,381,699.18

Makerere

2,681,979,857.83

402,296,978.67

Kipingo
Marinyi
Lupunga

149,318,982.00

126,431,856.76

Minepa

378,566,952.00

283,503,820.02

Mgolo

147405,751.78

147,405,751.78

Mkandarasi Mshauri

556,700,000

341,000,000

Jumla kuu

5,107,070,266.31

2,396,542,986

 

5.0 USAJILI WA VYOMBO HURU VYA WATUMIAJI MAJI (COWSOs)

Kulingana na sheria mpya ya maji ya mwaka 2009 miradi yote ya maji inabidi iundiwe vyombo huru vya watumiaji maji vitakavyopendekezwa na kukubaliwa na jamii husika kulingana na mwongozo na sheria za maji Na. 12 ya mwaka 2009.

Katika kutekeleza jukumu hilo Halmashauri imesha sajili Jumuiya za watumiaji maji 6 ambazo

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA ULANGA October 04, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI November 22, 2021
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA MFUMO WA ANUANI ZA MAKAZI TARAFA YA VIGOI March 14, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI YA MWAKA 2022 May 06, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Hakimu mfawidhi Ulanga atambulisha wiki ya sheria

    January 17, 2024
  • Hakimu mfawidhi Ulanga atambulisha wiki ya sheria

    January 17, 2024
  • Bonanza la Uhuru lafana Ulanga

    December 08, 2023
  • Kuelekea Siku ya 9 December Viongozi na Wananchi wa Wilaya ya Ulanga wafanya usafi katika Hospital ya Wilaya

    December 06, 2023
  • Angalia Zaidi

Video

Link Kuripoti shuleni
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Vipindi vya Radio Ulanga
  • Majukumu ya Viongozi wa Serikali za Mitaa
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA FFARS
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

    Anwani ya Posta: P.O. BOX 22

    Telephone: +2550232626340

    Simu: 0763845957

    Barua pepe: ded@ulangadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2017 Ulanga District Council . All rights reserved.