• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga
Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Eneo la Utawala
    • Majukumu ya Viongozi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi na Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Radio Ulanga FM
      • Ijue Radio Ulanga FM
      • Vipindi vya Radio Ulanga FM

kamati za ujenzi wilaya ya Ulanga watakiwa kusimamia mafundi ili kutekeleza miradi kwa wakati

Imetumwa: April 22nd, 2021

Na.Yuster Sengo

Mweyekiti Wa halmashauri ya wilaya ya wilaya ya Ulanga mh .Edson Solly Amezitaka kamati zote zinazosimamia miradi ya ujenzi wa maabara Za Shule Za Sekondari na madarasa kwa shule Za Msingi pamoja na ujenzi wa zahanati Za Vijiji kusimamia kwa ukaribu na umakini miradi Yote kwa kuwa wao ndio wasimamizi wakuu katika miradi hiyo

Hayo ameyesema kwa nyakati tofauti katika  ziara ya kamati ya fedha ,Utawala na mipango yakukagua miradi ya maendeleo iliyopatiwa fedha Za Utekelezaji ili kuona na kujiridhisha kazi zilizofanyika kutokana na fedha zilizotolewa katika miradi husika

Aidha amezitaka kamati hizo kusimamia mafundi wanaotekeleza miradi hiyo kwani mafundi hao wapo chini ya kamati hizo

“Kamati hakikisheni mna wasimamia mafundi kwenye utekelezaji wao kwakuwa wapo chini yenu ,Namnapooona kuwa kuna shida yoyote mtupe taarifa mapema ili tuone namna ya kufanya kabla Mambo Hayajaharibika. Amesemamh.Solly

“Hata hivyo nivizuri kwa Fundi Mkuu kutumia vibarua waliopo kwenye eneo La Mradi kwani itapunguza sana malalamiko kwakuwa mara nyingi hawa vibarua huwa wanafanya kazi Za Majitolea hapa sasa nivizuri Pia Kuwapa kazi ili na wao waweze kupata fedha kidogo” Ameongeza mh. Solly

Hata hivyo Mh .Solly aliwataka madiwani kusimamia na kuhamasisha wananchi katika majitoleo ya nguvu kazi ili miradi imalizike kwa wakati na kuokoa fedha zinazoelekezwa kwenye miradi hiyo na kuanzisha majengo mengine kwa pesa zinazobaki kwenye mradi husika

“Kukiwa na nguvu kazi Za Kutosha ,Maboma yanasimamishwa kwa muda mfupi na bila gharama,Hivyo tukipata fedha Za Umaliziaji zinakuwa zinatosha kabisa na zinzazobakia tunaweza kutelekeza kwenye ujenzi wa Jengo Lingine kama ambavyo wamefanya baadhi ya maeneo tuliyopita”Amesema Mh.Solly Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ulanga

“Na jambo linguine tuhakikishe wananchi wanaondoa siasa kwenye maeneo yao kwani kwa kufanya hivyo wanazorotesha maendeleo katika vijiji vyao “Ameongeza Mh.Solly

Kwa Upande Wake Diwani wa Lukande Mh .Novatus majiji alisema kuwa jamii inapaswa kushirikishwa katika miradi Yote Inapatiwa fedha Za Utekelezaji na serikali

“Nilazima jamii zetu zishirikishwe kwenye miradi ya maendeleo ili waweze kuchangia nguvu kazi na tukumbuke kwamba nguvu kazi hizi zinasaidia sana kwenye kuokoa pesa ambazo zinaweza kutekeleza miradi mingine ndani ya eneo husika”Amesema Mh.Majiji

Akizungumza katika kikao Cha Kamati ya fedha na mipango wakati wa kujadili taarifa ya ziara ya kamati ya fedha, Utawala na mipango mwenyekiti wa halamashauri ya wilaya ya  Ulanga Mh.Edson Solly Amemtaka mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ulanga ndg.Jonas Mallosa kuliangalia kwa jicho La Pili suala la Nguvu kazi katika kata ya Mahenge kwani kumeonekana Hakuna Kabisa nguvu kazi na badala yake miradi inatekelezwa kwa kutumia fedha kuanzia mwanzo wa mradi hadi kumalizia mradi

“Nikuombe mkurugenzi lifanyie kazi suala la nguvu kazi katika eneo hili La Mahenge,kwani sehemu nyingine ukiwapa milioni thelathini wanafanya na kazi za ziada,lakini hapa wataitumia yote na muda mwingine inaweza isitoshe kwakuwa hawatumii nguvu kazi kabisa “Amesema Mh.Solly

Aidha kwa upande wa mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ulanga Ndg .Jonas Mallosa amesema kuwa kazi zote zinafanyika vizuri kwasababu ya ushirikiano mkubwa baina ya menejimenti na madiwania mbao wamekuwa wakisimamia miradi hiyo kwa ukaribu ili iweze kuisha kwa wakati uliopangwa

“Na Pia Niwashukuru watu wasali pamoja na Gombe Kwani walikuwa nyuma sana lakini kwa sasa kutokana na ushirikiano uliokuwepo wanaendelea vizuri na inawezekana wakakamilisha kwa wakati uliopangwa “Amesema Ndg. Mallosa

Jumla ya miradi iliyokaguliwa na kamati ya fedha,Utawala na mipango ni miradi 16 Ambayo ni miradi ya umaliziaji wa ujenzi wa vyumba vya maabara katika shule Za Sekondari,Umaliziaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule Za Msingi pamoja na umaliziaji wa ujenzi wa zahanati Za Vijiji ,ambapo madiwani tisa na wataalam wa halmashauri walishiriki katika ziara hiyo ya siku mbili.


Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA ULANGA October 04, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI November 22, 2021
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA MFUMO WA ANUANI ZA MAKAZI TARAFA YA VIGOI March 14, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI YA MWAKA 2022 May 06, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Hakimu mfawidhi Ulanga atambulisha wiki ya sheria

    January 17, 2024
  • Hakimu mfawidhi Ulanga atambulisha wiki ya sheria

    January 17, 2024
  • Bonanza la Uhuru lafana Ulanga

    December 08, 2023
  • Kuelekea Siku ya 9 December Viongozi na Wananchi wa Wilaya ya Ulanga wafanya usafi katika Hospital ya Wilaya

    December 06, 2023
  • Angalia Zaidi

Video

Link Kuripoti shuleni
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Vipindi vya Radio Ulanga
  • Majukumu ya Viongozi wa Serikali za Mitaa
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA FFARS
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

    Anwani ya Posta: P.O. BOX 22

    Telephone: +2550232626340

    Simu: 0763845957

    Barua pepe: ded@ulangadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2017 Ulanga District Council . All rights reserved.