• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga
Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Eneo la Utawala
    • Majukumu ya Viongozi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi na Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Radio Ulanga FM
      • Ijue Radio Ulanga FM
      • Vipindi vya Radio Ulanga FM

Elimu ya Makuzi

Imetumwa: June 11th, 2018

ULANGA

Na

Fatuma Mtemangani

Mradi wa kinga dhidi ya maambukizi ya VVU na athari za UKIMWI kwa Wasichana balehe na Wanawake Vijana kutoka  Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Maendeleo ya Jamii) umezinduliwa Wilayani Ulanga mkoani Morogoro na mkuu wa wilaya ya Ulanga ndugu Jackob Joseph Kassema.

Mradi huo una lengo la kutoa mafunzo ya malezi na makuzi kwa wasichana balehe na wanawake vijana walioko shule na nje ya mfumo wa elimu,kutoa elimu ya ujasiriamali na stadi za maisha kwa walio nje ya mfumo wa elimu,kuwapatia pedi wasichana walioko shule na nje ya mfumo wa elimu,kutoa elimu ya kujikinga na maambukizi ya VVU kwa mikoa mitatu ikiwemo mkoa wa Dodoma,Singida na Morogoro.

Akizungumzia mafanikio yatakayo patikana ndani ya mradi huo kaimu mkurugenzi wa mradi huo bwana Mapunda amesema kua kwa mkoa wa morogoro mradi huo utatekelezwa katika wilaya ya Ulanga,Malinyi pamoja na Ifakara DC kwa kutoa elimu waelimishaji rika,wazazi wa wasichana balehe,kujikinga na maambukizi ya VVU ikiwemo upigaji wa simu na ujumbe mfupi bure ili kupata taarifa muhimu na usahihi.

Hata hivyo bwana Mapunda amesema kuwa  Mradi utatekelezwa katika kata na vijiji vyote ambavyo vimefikiwa na mpango wa TASAF wa kunusuru kaya maskini katika Halmashauri za Malinyi, Ulanga na Ifakara.

Mkuu wa Wilaya ya Ulanga ndugu Jackob Kassema ameshukuru mradi wa  kinga dhidi ya maambukizi ya VVU na athari za UKIMWI kwa Wasichana balehe na Wanawake Vijana katika Wilaya ya Ulanga kwani  Wilaya ya Ulanga ni Wilaya inayofanya vizuri kupitia miradi mbalimbali wanayopata.

Hivyo mkuu wa Wilaya ndug Kassema amewataka waanzilishi wa miradi hiyo kuwa endelevu ili iweze kusaidia kwa vizazi vya sasa na baadae kwani wananchi walio wengi hawana uelewa wa kutosha juu ya maambukizi ya VVU na athari za UKIMWI kwa Wasichana balehe na Wanawake Vijana

 “ Nawasihi wananchi wangu Hatari ya Maambukizi ya VVU kwa Wasichana Balehe na Wanawake Vijana hivyo kama mzazi au mlezi jenga tamaduni ya kuzungumza na motto wako wa kike ili asiingie kwenye vishawishi kabla ya umri wake kufikia na kukatisha ndoto zake”.

Hatari ya Maambukizi ya VVU kwa Wasichana Balehe na Wanawake Vijana yanachangiwa na sababu kuu 3 ambazo ni sababu za kitabia (behavioral), za kibaiolojia (biological) na mtambuka (structural),Umaskini wa kipato katika kaya unawaweka Wasichana Balehe na Wanawake Vijana katika hatari ya kupata maambukizi ya VVU kwa kushiriki ngono zisizo salama ili kupata kipato na Wasichana waliokatisha masomo hawapati  mbinu mbadala za kujikimu kimaisha zikiwemo stadi za maisha na ujasiriamali hivyo kuwa kwenye hatari ya kushiriki biashara ya ngono  ambayo ni kichocheo kikubwa cha maambukizi ya VVU

Aidha Kutokana na  kufanya ngono zisizo salama, kundi hili lipo kwenye hatari ya kupata mimba za utotoni, kuolewa katika umri mdogo na kufanyiwa vitendo vingine vya ukatili vinavyochangia uwezekano wa kupata maambukizi ya VVU.

Kutokana na changamoto hizo,Serikali kupitia usaidizi wa GF, imeamua kuanzisha na kuendeleza mpango wa VVU na UKIMWI kwa kundi la Wasichana Balehe na Wanawake Vijana ikiwemo Kubadili tabia,mpango wa upimaji wa VVU na matibabu ya UKIMWI,Afya ya Uzazi,kuondoa umaskini wa kipato na mtambuka.

Katika kupunguza umaskini wa kipato, mradi huu utalenga kaya maskini zaidi kama zitakavyokuwa zikiainishwa na mpango wa kunusuru kaya maskini inayoratibiwa na TASAF, kwa kutumia mfumo wa utoaji wa ruzuku kwa kaya maskini zaidi.

“Katika utekelezaji wa mpango huu, ni jukumu la Maafisa Maendeleo ya Jamii kuhakikisha kwamba miradi ya aina hii inaoanishwa na majukumu ya msingi ya kada ya Maendeleo ya Jamii ya kuelimisha, kuhamasisha na kuikinga jamii dhidi ya athari zinazotokana na harakati za kujitafutia maendeleo”.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA ULANGA October 04, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI November 22, 2021
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA MFUMO WA ANUANI ZA MAKAZI TARAFA YA VIGOI March 14, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI YA MWAKA 2022 May 06, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Hakimu mfawidhi Ulanga atambulisha wiki ya sheria

    January 17, 2024
  • Hakimu mfawidhi Ulanga atambulisha wiki ya sheria

    January 17, 2024
  • Bonanza la Uhuru lafana Ulanga

    December 08, 2023
  • Kuelekea Siku ya 9 December Viongozi na Wananchi wa Wilaya ya Ulanga wafanya usafi katika Hospital ya Wilaya

    December 06, 2023
  • Angalia Zaidi

Video

Link Kuripoti shuleni
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Vipindi vya Radio Ulanga
  • Majukumu ya Viongozi wa Serikali za Mitaa
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA FFARS
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

    Anwani ya Posta: P.O. BOX 22

    Telephone: +2550232626340

    Simu: 0763845957

    Barua pepe: ded@ulangadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2017 Ulanga District Council . All rights reserved.