• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga
Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Eneo la Utawala
    • Majukumu ya Viongozi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi na Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Radio Ulanga FM
      • Ijue Radio Ulanga FM
      • Vipindi vya Radio Ulanga FM

Kamishna jenerali wa magereza afanya ziara ya kihistoria katika gereza la Mahenge wilayani Ulanga

Imetumwa: January 9th, 2019

ULANGA

NA Fatuma Mtemangani

Kamishna jenerali wa Magereza Afande Phaustine Kasike amefanya ziara ya kihistoria katika gereza la Mahenge Wilayani Ulanga mkoani Morogoro na kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na gereza hilo.

Kamishna Jenerali Afande Kasike alipokelewa na mkuu wa gereza la Mahenge Afande Stockwell Mlyuka na kusomewa taarifa fupi ya kituo hicho na pia alipata nafasi ya kuongea na wafungwa pamoja na mahabusu wa gereza hilo ili kusikiliza shida na kero mbalimbali zinazowakabili.

Kamishna jenerali alikagua miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo zahanati,nyumba ya kufikia askari wageni[Rest House]hasa wanaotoka mafunzoni[Depo],Mabwawa ya samaki aina ya sato pamoja na uzalishaji wa Mifugo .

Pia kamishna jenerali amempongeza mkuu wa gereza la Mahenge Afande Stockwell Mlyuka kwa kazi nzuri anayoifanya kwa kubuni miradi mbalimbali ya maendeleo na kumtaka aendelee kubuni miradi mingine itakayosaidia jeshi na Taifa kwa ujumla kwani jeshi la gagereza lipo katika mpango wa kujitegemea hasa kwa upande wa chakula.

Hata hivyo kamishna jenerali Kasike alipata nafasi ya kuzungumza na maafisa na askari wa gereza hilo na kufurahia kuona wanafanya kazi kwa ushirikiano hivyo amewataka watumishi hao kuendeleza ushirikiano huo kwa mkuu wa gereza hilo kwa ajili ya kuleta maendeleo na pia kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake wafanye kazi kwa bidii,maarifa na weledi na kufuata kanuni na taratibu za jeshi la magereza japo kuna changamoto mbalimbali zinazoikabili jeshi la magereza tayari baadhi ya changamoto hizo zimeanza kupatiwa ufumbuzi.

“Nimefurahi sana kuona mnafanya kazi kwa kushirkikiana vizuri najua kuna changamoto nyingi zinawakabili jeshi la Magereza lakini kwa sasa baadhi ya changamoto hizo zinafanyiwa ufumbuzi na zingine zinaendelea kutafutiwa ufumbuzi hivyo mnapaswa kufanya kazi kwa kufuata kanuni na taratibu za jeshi la Magereza na muache kufanya kazi kwa mazoea.”Alisema kamishna jenerali Kasike.

Aidha amewataka watumishi wa jeshi la Mgereza Mahenge kujiepusha na vitendo vya kupokea au kutoa rushwa na yeyote atakaebainika anafanya vitendo hivyo kinyume na maadili ya jeshi la magereza atachukuliwa hatua kali za kinidhamu ikiwa na kufukuzwa kazi.

Kwa upande wake mkuu wa gereza hilo Afande Stockwell Mlyuka amemuahidi kamishna jenerali Kasike kutomuangusha na ataendelea kufanya kazi kwa kufuata kanuni na taratibu za jeshi la magereza hivyo hatomuonea aibu asakari yeyote atakaekiuka maadili ya jeshi la magereza,pia kuendelea kubuni miradi mbalimbali ya maendeleo katika gereza hilo.

Katika ziara hiyo kamishna jenerali Kasike aliongozana na kamanda wa magereza wa mkoa wa Morogoro afande Silvester Mrema pamoja na maofisa wengine wa jeshi la magereza.

Kamishna jenerali Phaustine Kasike ameahidi kutembelea vituo vyote vilivyo pembezoni ikiwemo gereza la Mahenge ambapo Kumbukumbu za gereza hilo zinaonesha kuwa halikuwahi kutembelewa na mkuu wa jeshi la magereza tangu kuanzishwa kwake mwaka 1886 hivyo ziara ya kamishna jenerali Kasike imekuwa ni ya kihistoria katika gereza la Mahenge lililopo Wilayani Ulanga mkoani Morogoro.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA ULANGA October 04, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI November 22, 2021
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA MFUMO WA ANUANI ZA MAKAZI TARAFA YA VIGOI March 14, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI YA MWAKA 2022 May 06, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Hakimu mfawidhi Ulanga atambulisha wiki ya sheria

    January 17, 2024
  • Hakimu mfawidhi Ulanga atambulisha wiki ya sheria

    January 17, 2024
  • Bonanza la Uhuru lafana Ulanga

    December 08, 2023
  • Kuelekea Siku ya 9 December Viongozi na Wananchi wa Wilaya ya Ulanga wafanya usafi katika Hospital ya Wilaya

    December 06, 2023
  • Angalia Zaidi

Video

Link Kuripoti shuleni
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Vipindi vya Radio Ulanga
  • Majukumu ya Viongozi wa Serikali za Mitaa
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA FFARS
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga

    Anwani ya Posta: P.O. BOX 22

    Telephone: +2550232626340

    Simu: 0763845957

    Barua pepe: ded@ulangadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2017 Ulanga District Council . All rights reserved.